Skip to main content

Athletico yafa 'kisabuni' yaichapa 2-1 Real Madrid

Mchezo wa marudiano nusu fainali ya ligi ya mabingwa ulaya kati ya Athletico Madrid na Real Madrid umemalizika hii leo kwa Athletico Madrid kuchomoza na ushindi wamagoli 2 kwa 1 dhidi ya Real Madrid.

Athletico ndio waliokuwa wa kwanza kupata magoli yote mawili kupitia kwa Saul Niguez dakika ya 13 baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliochongwa na Koke.
Saul Niguez akiipatia Athetico Madrid goli la kwanza kwa kichwa
Athletico walipata goli la 2 kwa njia ya penalt kupitia kwa Antoine Griezmann baada ya Fernando Torres kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari la madrid.
Mpira uliendelea kwa kasi huku Madrid wakianza kulikaribia lango la Athletico kwa mara nyingi zaidi na
kunako dk ya 43 Isco Alarcon aliipatia Madrid bao la kufuta machozi baada ya shughuli pevu ya Karim Benzema kuwatambuka wachezaji 3 wa Athletico na kutoa pasi kwa Kroos ambaye shuti lake lilipanguliwa na Oblak kabla ya Isco kumalizia.
Mpaka timu zinaenda kwa mapumziko, Athletico 2-1 Madrid.Kipindi cha pili kilianza kwa mpira kuanza kutawaliwa zaidi na wageni Real Madrid ambao licha ya kushindwa kuongeza goli la pili, walifanya mashambulizi ya hatari langoni mwa wapinzani wao ikiwemo mpira uliotiwa nyavuni na Cristiano Ronaldo ambao mwamuzi aliamuru kuwa Ronaldo alikuwa ameshaotea.
Mpaka mwamuzi anapuliza kipenga cha mwisho, Athletico 2-1 Real Madrid. Kufuatia matokeo haya Real Madrid wanatinga fainali na watakutana na Juventus ambao walitangulia hapo jana baada ya kuwaondosha Monaco. Real Madrid atakuwa anatafuta nafasi ya kuutetea ubingwa wake baada ya kulinyakuwa tena kombe hili mwaka jana.


Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...