Skip to main content

Bale Huyooo Manchester United

Gareth Bale amekubali kujiunga na klabu ya Manchester United mwishoni mwa msimu huu kwa masharti kuwa klabu hiyo sharti ifuzu michuano ya ligi ya Mabingwa msimu ujao.
Inasemekana Bale amefikia makubaliano ya awali na Manchester United na yupo tayari kuachana na La liga kutokana na sintofahamu inayomkabili huku jarida la Diaro Gol likisema kuwa Rais wa klabu hiyo Fiorentino Perez amechoshwa na hali ya majeruhi yanayomkabili kila mara.
 Bale amekuwa akisumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara na amefanikiwa kuanza katika michezo 24 tu msimu huu huku akianza katika michezo 17 tu ya La liga na kupachika jumla ya magoli 9. Hali kwa Bale imekuwa mbaya zaidi pale ambapo wachezaji wanaochukua nafasi yake kama Isco, Marco Asencio na James Rodriguez wakionekana kuitendea haki nafasi hiyo.
Manchester United wapo nafsi ya 5 katika msimamo wa ligi ya EPL huku wakiwa na matumaini machache ya kumaliza katika nafasi ya nne. Hata hivyo matumaini yao yamesalia katika michuano ta Uefa Europa ambapo kwasasa wapo kwenye hatua ya nusu fainali dhidi ya Celta De Vigo na tayari wameshacheza mchezo wa kwanza ambapo Mancheaster United ilitoka kifua mbele ugenini kwa ushindi wa goli 1-0.

Mechi ya marudiano itapigwa Old Trafford kesho jumatano huku kukiwa na kila dalili kuwa Manchester United watafuzu hatua hiyo na wanatabiriwa kukutana na Ajax katika fainali kutokana na matokeo mazuri ya awali Ajax waliyoyapata. Ajax walishinda mchezo wao wa kwanza wakiwa nyumbani Amsterdam kwa magoli 4-1 dhidi ya Lyon. Shukrani za dhati kwa mchezaji wa Chelsea anayekipiga kwa mkopo Ajax Betrand Traore kwa kupachika magoli 2.
Fainali ya kombe la EUROPA itapigwa katika mji wa Stockholm, nchini Sweden.

Na Walter Stephen.  



Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...