Skip to main content

MAHREZ: Nataka kuondoka Leicester City

Mchezaji bora wa mwaka jana wa ligi kuu ya Uingereza Riyad Mahrez amesema anataka kuondoka Leicester City msimu huu wa majira ya joto.
Mahrez amesema kuwa amekuwa na shauku ya kuendeleza soka lake sehemu nyingine na walikubaliana na klabu kuwa angesalia hapo King Power kwa mwaka mmoja tu hivyo muda umekwisha.

Mualgeria huyo mwenye umri wa miaka 26 aliisaidia Leicester City kunyakua ubingwa  wa Premier League msimu uliopita wa mwaka 2015/2016.
Mahrez pia ameisaidia timu hiyo kusalia katika ligi kuu msimu huu kwa kupachika wavuni magoli 10, baada ya kusuasua katika michezo ya mzunguko wa kwanza wa ligi lakini kama haitoshi pia ameisaidia kufika hadi hatua ya robo fainali katika michuano ya ligi kuu ya mabingwa ulaya.

"Pamoja na kuwa naihusudu na kuiheshimu Leicester City, napenda kuwa mkweli na muwazi. Nimeongea na klabu yangu na nimewaambia kuwa nadhani sasa ni muda muafaka wa kuendelea mbele" Mahrez alisema.

"Nimekuwa na maongezi mazuri tu na mwenyekiti msimu uliopita na tulikubaliana kwa muda ule kuwa nitakaa kwa mwaka mmoja mwingine ili niisaidie timu yangu kwa nguvu zote kufuatia kipindi cha mpito toka kubeba ubingwa na kucheza Champions League".

"Nimekuwa na misimu minne mizuri na Leicester na nimefurahia kila wakati nilipokuwa hapa. Najihisi mwenye ufahari mkubwa kuwa sehemu ya mafanikio tuliyoyapata nikiwa hapa, ikiwemo kuwa mabingwa wa ligi kuu.
"Mahusiano niliyoshea na klabu na mashabiki hawa wazuri, ni moja ya vitu nitakavyovikumbuka milele na naamini wataelewa na kuheshimu maamuzi yangu". Alimalizia Mahrez ambaye alisajiliwa na Leicester mwaka 2014 akitokea Le Harve ya Ufaransa.


TUFUATILIE KUPITIA FACEBOOK NA TWITTER

Bofya hapa chini ku-like ukurasa wetu wa facebook
https://www.facebook.com/RadaYetuSports/

Bofya hapa kutufuatilia kupitia twitter
https://twitter.com/RadaYetu


Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...