Na walter stephan
Mchezo wa awamu ya kwanza wa nusu fainali ya ligi mabingwa ulaya baina ya Real madrid na Athletico madrid ulimalizika kwa Mchezaji bora wa dunia kwa sasa Cristiano Ronaldo kudhihirisha ubora wake katika michuano hiyo baada ya kufunga magoli yote 3 ambayo timu yake iliyapata.
Mchezo huo ulianza kwa kasi ya kuridhisha na Katika dk ya 7 Carvajal aligongeana pasi vizuri na Isco katika lango la athletico kabla ya kufanya jaribio lililopanguliwa na mlinda mlango Oblak na kumbabatiza benzema ambaye alishindwa kuweka mpira ule kimiani.
Real Madrid ilianza kupata goli la kwanza kupitia kwa Cristiano Ronaldo dk ya 10 baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira ulioingizwa eneo la goli la athletico Madrid na carvajal.
Madrid waliendelea kuutawala mpira licha ya nafasi nzuri ya kusawazisha kwa upande wa athletico kupitia kwa Kelvin Gameiro kukataliwa vizuri na mlinda mango wa Real Madrid Kylor Navas.
Katika dk ya 29 benzema aliunganisha Mpira wa tik taka baada ya kazi nzuri ya kuwatambuka mabeki kufanywa na Ronaldo hata hivyo kazi hiyo ya hatari haikuzaa matunda kwa Mpira kupitia sentimita chache juu ya lango la wapinzani wao.
Hadi timu hizo zinaenda mapumziko Real Madrid walikuwa wako mbele kwa goli 1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kupooza kiasi huku Athletico wakijaribu kuuweka mpira kwenye himaya yao. Real Madrid iliongeza uhakika wa ushindi dk ya 73 baada ya Ronaldo kuiandikia goli la pili Madrid na goli lake la 102 katika michuano hiyo baada ya kupokea mpira kwa benzema na kupiga shuti Kali lililomshinda mlinda mlango wa athletico Madrid.
Ronaldo alikamilisha karamu ya hat-trick kunako dakika ya 86 baada ya kumalizia jitihada kubwa ya Lucas Vazquez aliyerudisha uwanjani Mpira uliokuwa unataka kutoka nje katika lango la watani wao. Hadi kipenga cha mwisho Real Madrid 3, Athletico Madrid 0.
Ronaldo amekuwa mwiba mkali kwa watani wao wa jadi kwani katika mchezo wa ligi ya Hispania mzunguko wa kwanza, Ronaldo aliwafunga tena Athletico hat-trick na kumfanya awe amewafunga jumla ya magoli sita kwa msimu huu.
Mchezo wa Marudiano utapigwa wiki ijayo siku ya jumatano katika uwanja wa Vicente Calderon katika mji huo huo wa Madrid, wakati huo ambapo Athletico Madrid watakuwa nyumbani.
Mchezo wa awamu ya kwanza wa nusu fainali ya ligi mabingwa ulaya baina ya Real madrid na Athletico madrid ulimalizika kwa Mchezaji bora wa dunia kwa sasa Cristiano Ronaldo kudhihirisha ubora wake katika michuano hiyo baada ya kufunga magoli yote 3 ambayo timu yake iliyapata.
Mchezo huo ulianza kwa kasi ya kuridhisha na Katika dk ya 7 Carvajal aligongeana pasi vizuri na Isco katika lango la athletico kabla ya kufanya jaribio lililopanguliwa na mlinda mlango Oblak na kumbabatiza benzema ambaye alishindwa kuweka mpira ule kimiani.
Real Madrid ilianza kupata goli la kwanza kupitia kwa Cristiano Ronaldo dk ya 10 baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira ulioingizwa eneo la goli la athletico Madrid na carvajal.
Madrid waliendelea kuutawala mpira licha ya nafasi nzuri ya kusawazisha kwa upande wa athletico kupitia kwa Kelvin Gameiro kukataliwa vizuri na mlinda mango wa Real Madrid Kylor Navas.
Katika dk ya 29 benzema aliunganisha Mpira wa tik taka baada ya kazi nzuri ya kuwatambuka mabeki kufanywa na Ronaldo hata hivyo kazi hiyo ya hatari haikuzaa matunda kwa Mpira kupitia sentimita chache juu ya lango la wapinzani wao.
Hadi timu hizo zinaenda mapumziko Real Madrid walikuwa wako mbele kwa goli 1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kupooza kiasi huku Athletico wakijaribu kuuweka mpira kwenye himaya yao. Real Madrid iliongeza uhakika wa ushindi dk ya 73 baada ya Ronaldo kuiandikia goli la pili Madrid na goli lake la 102 katika michuano hiyo baada ya kupokea mpira kwa benzema na kupiga shuti Kali lililomshinda mlinda mlango wa athletico Madrid.
![]() |
Ronaldo akipiga mkwaju na kufunga goli la pili |
Ronaldo alikamilisha karamu ya hat-trick kunako dakika ya 86 baada ya kumalizia jitihada kubwa ya Lucas Vazquez aliyerudisha uwanjani Mpira uliokuwa unataka kutoka nje katika lango la watani wao. Hadi kipenga cha mwisho Real Madrid 3, Athletico Madrid 0.
Ronaldo amekuwa mwiba mkali kwa watani wao wa jadi kwani katika mchezo wa ligi ya Hispania mzunguko wa kwanza, Ronaldo aliwafunga tena Athletico hat-trick na kumfanya awe amewafunga jumla ya magoli sita kwa msimu huu.
Mchezo wa Marudiano utapigwa wiki ijayo siku ya jumatano katika uwanja wa Vicente Calderon katika mji huo huo wa Madrid, wakati huo ambapo Athletico Madrid watakuwa nyumbani.
Comments
Post a Comment