Klabu
ya Manchester City imethibitisha kuachana na wachezaji wake 5 wakiwemo
Jesus Navas, Gael Clichy, Bacary Sagna, Pablo Zabaleta na Willy Caballero.
Wachezaji hao mikataba yao inaisha msimu huu na klabu haiko tayari kuwaongezea mkataba mpya.
Tofauti na wengine, Zabaleta alithibitishwa mapema wiki hii kua angeondoka City huku wengine wakijua hatima yao leo hii.
Clichy alijiunga na Manchester City mwaka 2011 akitokea Arsenal na amebeba makombe manne akiwa na Manchester City ikiwemo la ligi kuu 2012 na 2014 na Kombe la ligi mwaka 2014 na 2016.
Navas aliyesajiliwa mwaka 2014 alifanikiwa kubeba makombe matatu yakiwemo hayo mawili ya Kombe la ligi na la ligi kuu 2014.Tayari klabu ya Valencia wameonyesha nia ya kumsajili mhispania huyo.
Wachezaji hao mikataba yao inaisha msimu huu na klabu haiko tayari kuwaongezea mkataba mpya.
Tofauti na wengine, Zabaleta alithibitishwa mapema wiki hii kua angeondoka City huku wengine wakijua hatima yao leo hii.
Clichy alijiunga na Manchester City mwaka 2011 akitokea Arsenal na amebeba makombe manne akiwa na Manchester City ikiwemo la ligi kuu 2012 na 2014 na Kombe la ligi mwaka 2014 na 2016.
Navas aliyesajiliwa mwaka 2014 alifanikiwa kubeba makombe matatu yakiwemo hayo mawili ya Kombe la ligi na la ligi kuu 2014.Tayari klabu ya Valencia wameonyesha nia ya kumsajili mhispania huyo.
Kwa upande wa Zabaleta ambaye yeye na Kompany ndio
wachezaji waliokaa Man City kwa muda mrefu kwa wachezaji waliopo mpaka
sasa, naye anaondoka huku klabu ya West Ham wakiwa njiani kukamilisha
usajili wa kumpokea mkongwe huyo muda wowote.
Pablo alisajiliwa akitokea
klabu ya Espanyol ya nchini Hispania mwaka 2008 na mpaka sasa
ameichezea City jumla ya mechi 230 za ligi kuu pekee ukiachia michuano mingine.
Caballero
yeye alisajiliwa na City mwaka 2014 na alikuwa langoni katika fainali
ya Kombe la ligi dhidi ya Liverpool 2016 ambapo wakuwa mabingwa. Amekuwa
akihudumia kama mlinzi wa akiba wa Man City kutokana na ubora wa kipa
namba moja Joe Hart ambaye baada ya ujio wa Guardiola alitolewa kwa
mkopo kwenda Torino.
Ujio wa Guardiola uliambatana na ujio wa mlinda lango wa Barcelona Claudio Bravo ila makosa
ya kipa huyo langoni ambaye alikuwa chaguo la kwanza la Pep Guardiola
mwanzo mwa msimu, yalimfanya Caballero kufurahia muda zaidi langoni kipindi cha ungwe ya pili ya
ligi kuu msimu huu. Mlinzi huyo anaachana na City angali akiwa kwenye jitihada za kuomba kusalia klabuni hapo.
Naye
beki wa kulia wa timu hiyo Bacary Sagna amethibitishwa kuondoka klabuni
hapo akiwa ameitumikia kwa misimu mitatu tu. Sagna alisajiliwa majira
ya joto mwezi July 2014 akitokea Arsenal na ameichezea City jumla ya
mechi 85.
Kwa
upande wa Yaya Toure ambaye alizungumziwa kuachana na klabu hiyo, hali
inaonekana huenda akaendelea kuitumikia. Habari ambazo hazijathibitishwa
na klabu yake ni kwamba Toure amepewa tena mkataba wa mwaka mmoja wa
kuitumikia.
Kati ya wachezaji sita (6) wa City waliozungumziwa kuondoka
kutokana na mikataba yao kuisha mwisho mwa msimu huu, Toure atakuwa
mchezaji pekee aliye bahatika kusalia endapo ni kweli amesaini mkataba
huo.
Comments
Post a Comment