Skip to main content

Usajili wa Paul Pogba kwenda Manchester Utata mtupu, FIFA kuuchunguza

Usajili wa kiungo Mfaransa Paul Pogba uliovunja rekodi ya dunia mwaka jana akitokea Juventus kwenda Manchester United unatarajiwa  kuchunguzwa na Shirikisho la soka duniani FIFA.
Dili hilo lililohusisha kitita cha paundi milioni 89 limegubikwa na taarifa zinazokinzana na taratibu za usajili zinazomhusisha wakala wa mchezaji huyo Mino Raiola.

Raiola anashukiwa kwa kosa la kusimamia usajili huo kwa kufanya kazi hiyo kama mhusika upande wa wanunuzi, na kwa wakati huo huo akisimamia upande wa wauzaji na hivyo kumfanya awe amehusika kwa pande tatu za usajili huo kutokana na yeye kuwa tayari ni wakala wa Pogba. Kwa mujibu wa taratibu za FIFA jambo hilo halikubaliki isipokuwa kwa sababu maalumu ambazo zinatakiwa ziwafikie FIFA.
Taarifa hizo zimetolewa na kitabu kilichochapiswa nchini ujerumani chenye kichwa cha habari "The Dirty Business in Football" ikimaanishwa "Madudu yanayofanyika kwenye biashara ya Mpira" kinachoandikwa na waandishi wa habari wawili wa Ujerumani na hutoka kwa awamu.

Inasemekana kuwa katika usajili huo uliomfanya Raiola kunufaika kwa kufanya majukumu matatu ulimpelekea kukubaliana na Manchester United kulipwa kitita cha paundi milioni 41 huku sehemu ya fedha hiyo ikilipwa kwa awamu.

Mpaka sasa si Pogba wala Raiola aliyezungumzia sakata hilo, na waandishi walipomhoji Raiola, alisema swala lake linashughulikiwa na wakili wake na hivyo hayupo tayari kulitolea ufafanuzi wowote.

Kocha wa Machester Jose Mourinho amesema hii leo kuwa, sakata hilo halitamathiri Pogba kwa sasa ambaye yeye na wachezaji wenzake wanajifua kuwakabili Celta Vigo kukamilisha ungwe ya nusu fainali ya kombe la Europa
usiku majira ya saa 6 pale Old Trafford.

Pogba anaitumikia Manchester United kwa awamu ya pili sasa alisajiliwa kutoka Juventus baada ya awali kununuliwa na vibibi vizee hio vya Turin (Juventus) akitokea hapo hapo Old Trafford.
Kabla ya kuitumikia Manchester kwa mara ya kwanza, Pogba alisajiliwa kutoka klabu ya Le Harve inayoshiriki ligi daraja la pili Ufaransa yaani French League 2.

Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...