Skip to main content

Yaya Toure kuwaaga mashabiki Etihad Jumanne ya kesho?

Kiungo wa Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast Yaya Toure (33) huenda akacheza mchezo wake wa mwisho katika dimba la Etihad wakati timu yake ikiwakabili West Bromwich Ablion na hivyo kuwa siku ya kuwaaga mashabiki wa Man City.
Matumaini ya Toure kusalia na Manchester City hayaonikani kutokana na kubakisha wiki chache katika mkataba wake huku kukiwa hakuna maongezi yoyote kati yake na meneja Pep Guardiola juu ya kusaini mkataba mpya.
Toure ambaye ni kipenzi cha mashabiki wa Manchester City amekataa ofa kadhaa za kuachana na klabu hiyo wakati akiwa hana maelewano mazuri na Guardiola lakini inaonekana huenda mechi ya jumanne akaitumia kuwaaga mashabiki kama hali itaendelea kubaki kama sasa.
Katika kipindi cha mwanzo wa msimu, kocha Giardiola aliacha kumchezesha mchezaji huyo mechi kadhaa na zaidi aliacha kumjumuisha katika kikosi ambacho kingeshiriki michuano ya UEFA. Hali hiyo ilimkwaza wakala wa mchezaji huyo Dimitri Seluk ambaye alifikia hatua ya kurushiana maneno na Guardiola huku Seluk akisema klabu hiyo itapoteza mashabiki katika bara la Afrika.
Kitendo cha kocha huyo kutompa nafasi kilitafsiriwa kuwa ni mwendelezo kocha huyo wa kuonyesha kuwa Toure halandani na mipango yake kwani akiwa kocha wa Barcelona alimuuza kwenda Manchester City kwa dau la paundi Mil.24 mwaka 2010
Pamoja na hali hiyo Toure alizidi kushikilia msimamo wake wa kutaka kubakia Etihad huku Guardiola akimtaka kumuomba radhi kwa kosa la wakala wake na baada ya muda Toure alimuomba radhi na ndipo alijumuishwa kwa mara ya kwanza katika mchezo dhidi ya Crystal Palace.

Katika mchezo huo Toure aliwadhihirishia mashabiki kiasi gani kocha alikosea kumuacha kwani aliipatia Man City magoli 2 na kupelekea mashabiki wachache kushangilia hadi kuingia uwanjani.
Kwasasa timu kadhaa zinawinda saini ya kiungo huyo zikiwemo, Westham, Newcastle na Brighton Albion na Inter Milan.
 

Baadhi ya mashabiki wa Manchester City walioingia uwanjani kushangilia na wachezaji wa timu hiyo baada ya Toure kufunga goli la ushindi

Askari wa Uwanjani wakujaribu kuwaondosha mashabiki walioingia uwanjani kushangilia goli la Yaya Toure lililofungwa dk ya 83

Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...