Skip to main content

Golden State Warriors wanyakuwa ubingwa wa NBA 2017

Ligi ya kikapu nchini marekani maarufu kama NBA imemalizika hii leo kwa timu ya Goldern State Warriors kubeba ubingwa mbele ya wapinzani wao Cleveland Caverliers kwa alama 4-1.
Katika fainali hiyo ambayo ilikuwa ni ya 5, Warriors wamepata ushindi wa pointi 129 dhidi ya 120 za Caverliers na kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa NBA kwa msimu wa 2016/2017.
Ushindi huu unahitimishwa kwa fainali 5 tu kati ya 7 zilizopangwa kutokana na Warriors kuwa mbele kwa michezo 4 dhidi ya Cavs walioshinda mchezo 1 jambo linalowafanya Warriors wasiweze tena kufikiwa na Cavs hata kama wangepoteza michezo miwili iliyosalia.
Staa wa Goldern State Warriors Kelvin Durrant, ametajwa kuwa mchezaji bora wa fainali za mwaka huu 2017 za NBA (NBA final MVP Player 2017) ikiwa ni msimu wake wa kwanza kuichezea Warriors baada ya kusajiliwa mwezi June 2016 akitokea Oklahoma City Thunders
Durrant ameonekana kustahili tuzo hiyo baada ya kutoa mchango mkubwa zaidi kwa Warriors katika ubingwa huu, kwa kufunga pointi zaidi ya 30 katika fainali zote 5. Durrant amefunga pointi 38, 33, 31, 35 na 39 katika fainali ya NBA mwaka huu.
PICHA ZA MATUKIO YA FAINALI YA NBA 2017
Staa wa Cavs LeBron James akipamuacha Durrant na kupachika mpira kwenye kikapu

Andre Iguodala wa Goldern State Warriors aki-dunk na kufunga dhidi ya Cavs

Stephen Curry akishangilia na mwanae baada ya ushindi

Kelvin Durrant wa Goldern State Warriors akishangilia mbele ya Kyrie Irving Caverliers

Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...