
Jarida la La Gazzetta dello Sport limeripoti kuwa maafikiano na miamba hiyo ya Italia imefikiwa leo, kwa mkroatia huyo aliyeifungia magoli 11 klabu yake ya Inter Milan na kutoa pasi za mwisho 11 msimu huu ulioisha.
Inter Milan wanalazimika kumuuza Perisic ndani ya mwezi June ili kuendana sambamba na matakwa ya UEFA kupitia sheria yake ya FFP(Financisl Fair Play Regulation) inayodhibiti matumizi ya fedha kwa vilabu kwenye kufanya usajili.
Chombo hicho kinachovitaka vilabu kutokufanya matumizi katika usajili, yanayozidi mapato ambayo klabu inayapata kimeilazimu Inter Milani kukubali kumruhusu Perisic kuondoka klabuni hapo akiwa ni kati ya wachezaji walioonyesha kiwango cha juu kwa msimu uliomazilika.
Perisic alisajiliwa na Inter Milan akitokea Wolfsburg ya nchini Ujerumani mwaka 2015 na katika timu hizo mbili alizozitumikia, zote amezifungia idadi sawa ya magoli ambayo ni 18.
Pia amewahi kuzichezea timu nyingine kama Borrusia Dortmund ya ujerumani na Club Brugge ya Ubelgiji.
Comments
Post a Comment