Skip to main content

Rufaa ya Athletico Madrid kupinga kuzuiwa kusajili yatupiliwa mbali


Mahakama ya Usuluishi wa Michezo yaani "Court of Abbritration for Sports" CAS imetupilia mbali rufaa iliyowasilishwa na klabu ya Athletico Madrid kutoka nchini Hispania dhidi ya FIFA ya kupinga kunyimwa kusajili msimu huu.
Athletico Madrid walikata rufaa hiyo kufuatia adhabu waliyopewa mwezi Julai 2016 na shirikisho la soka duniani FIFA ya kutosajili mchezaji mpya kwa madirisha mawili ya usajili yaani Januari 2017 na Julai 2017 mwaka huu pamoja na kulipa faini ya Paundi 719,793.
Adhabu hii walipewa kufuatia kuvunja sheria za FIFA zinazohusu usajili kwa wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 18.
Athletico Madrid aliadhibiwa kipindi kimoja na mahasimu wao Real Madrid kwa makosa yanayofanana ila rufaa ya Real Madrid iliyowasilishwa kwa CAS mwaka jana ilikubaliwa mwezi Desemba 2016 kwa kupunguziwa adhabu ya kutosajili kwa kipindi cha dirisha dogo la Januari tu.
Hali hiyo iliwafanya Real Madrid kutumikia adhabu yao kwa mwezi wa Januari na hivyo kuruhusiwa kuendelea na usajili wa wachezaji wapya katika kipindi hiki cha usajili (July 2017)
Pamoja na kukataliwa kwa rufaa ya Athletico madrid, wamepunguziwa adhabu ya faini waliyotakiwa kulipa kutoka  Paundi. 719,793 hadi paundi 439,873.
Kufuatia taarifa hii Athletico Madrid itaathirika kwenye mbio za kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa na timu ya Lyon, Alexandre Lacazette ambaye tangu awali aliweka wazi kuwa Athletico Madrid ndiyo sehemu anayodhani kuwa ni sahihi kuendelezea soka lake na tayari miamba hiyo kutoka Vicente Calderon walishaanza mbio za kumuwania.
Taarifa hii pia huenda ikawa mbaya kwa kocha Jose Mourinho na klabu ya Manchester United waliokuwa wakimuhitaji mshambuliaji wa Athletico Madrid, Antoine Griezmann kwani huenda Athletico wakaanza mazungumzo ya kumuomba asiondoke ingawa makubaliano ya mkataba yalikuwa yanamruhusu Griezmann kuondoka msimu huu.
Taarifa hii pia huenda ikawa njema kwa Liverpool waliokuwa wakiwania saini la Lacazzette ingawa Arsenal pia imeingia katika mbio hizo hasa baada ya kutoka kwa taarifa hii.

Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...