Skip to main content

Ratiba nzima ya Arsenal msimu wa Premier League 2017/2018

The Gunners wataanza msimu kwa kuwakaribisha mabingwa wa mwaka jana Leicester City katika uwanja wao wa Emirates.
Arsenal ambao kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 21 wameshindwa kumaliza ligi katika nafasi nne za juu, watahitaji kuzichanga vyema karata zao ili kurejea kwenye makali huku Kocha Arsene Wenger akionekana kuwa bize kwenye usajili huu, huku akiwa tayari ameshaanza kusajili kwa kumsajili beki Kolasinac kutoka Shalke04.
Ndani ya mwezi huohuo wa August, Arsenal watakutana na Liverpool, waliowapokonya nafasi ya nne na pengine wakatumia mchezo huo ambao ndio mechi kubwa ya kwanza, kuonyesha namna walivyojipanga msimu huu.
Liverpool iliwafunga Arsena katika michezo yote miwili ya ligi kuu msimu uliopita, huku wakigombania nafasi ya nne katika mechi za lala salama.
Ungwe ya mwisho itawashuhudia washika mitutu hao wakiwa ugenini kuwakabili Huddersfield Town waliopanda daraja.
TAREHEMUDA MECHI
12/08/2017 15:00 Arsenal v Leicester City
19/08/2017 15:00 Stoke City v Arsenal
26/08/2017 15:00 Liverpool v Arsenal
09/09/2017 15:00 Arsenal v Bournemouth
16/09/2017 15:00 Chelsea v Arsenal
23/09/2017 15:00 Arsenal v West Bromwich Albion
30/09/2017 15:00 Arsenal v Brighton and Hove Albion
14/10/2017 15:00 Watford v Arsenal
21/10/2017 15:00 Everton v Arsenal
28/10/2017 15:00 Arsenal v Swansea City
04/11/2017 15:00 Manchester City v Arsenal
18/11/2017 15:00 Arsenal v Tottenham Hotspur
25/11/2017 15:00 Burnley v Arsenal
28/11/2017 19:45 Arsenal v Huddersfield Town
02/12/2017 15:00 Arsenal v Manchester United
09/12/2017 15:00 Southampton v Arsenal
12/12/2017 19:45 West Ham United v Arsenal
16/12/2017 15:00 Arsenal v Newcastle United
23/12/2017 15:00 Arsenal v Liverpool
26/12/2017 15:00 Crystal Palace v Arsenal
30/12/2017 15:00 West Bromwich Albion v Arsenal
01/01/2018 15:00 Arsenal v Chelsea
13/01/2018 15:00 Bournemouth v Arsenal
20/01/2018 15:00 Arsenal v Crystal Palace
30/01/2018 19:45 Swansea City v Arsenal
03/02/2018 15:00 Arsenal v Everton
10/02/2018 15:00 Tottenham Hotspur v Arsenal
24/02/2018 15:00 Arsenal v Manchester City
03/03/2018 15:00 Brighton and Hove Albion v Arsenal
10/03/2018 15:00 Arsenal v Watford
17/03/2018 15:00 Leicester City v Arsenal
31/03/2018 15:00 Arsenal v Stoke City
07/04/2018 15:00 Arsenal v Southampton
14/04/2018 15:00 Newcastle United v Arsenal
21/04/2018 15:00 Arsenal v West Ham United
28/04/2018 15:00 Manchester United v Arsenal
05/05/2018 15:00 Arsenal v Burnley
13/05/2018 15:00 Huddersfield Town v Arsenal

Comments

Popular posts from this blog

Wajue Wafungaji bora wa EPL kwa kila timu inayoshiriki sasa

1. CHELSEA - Frank Lampard -147 Lampard ndiye anayeshikilia rekodi ya mfungaji bora wa Chelsea wa muda wote yaani tangu (Chelsea) ilipoanzishwa akitupia kambani magoli 211. Alisajiliwa akitokea West ham mwaka 2001 na kwa sasa ni moja kati ya mashujaa wa kubwa wa klabu ya Chelsea. Alifunga goli la kwanza la Premier League akiwa na Chelsea December 23, 2001. Goli la mwisho alilifunga 05 April 2014. 2. TOTTENHAM - Teddy Sheringham - 98 Teddy Sheringham anafahamika kama "Legend" wa Tottenham Hotspurs pamoja na kuvichezea vilabu takribani 10 vya nchini uingereza ikiwemo Manchester United na West ham United. Alisajiliwa na Tottenham akitokea Nottingham Forest mwaka 1992 na alisajiliwa na Man United 1997 kabla ya kurejea tena Tottenham 2001. Aliifungia Spurs goli la kwanza tar.02.september 1992 na la mwisho tar. 21 April 2003 kabla hajatimkia Portsmouth   3. MANCHESTER CITY - Sergio Aguero -120 Akiwa amesaliwa na magoli 10 tu kuwa mfungaji bora wa historia wa M...

Liverpool kuwakumbuka 96 waliokufa janga la Hillsborough: Ifahamu zaidi "HILLSBOROUGH DISASTER"

Familia ya wana Liverpool FC wakiwemo wakiwemo mashabiki, wachezaji, Viongozi wa timu pamoja na wanafamilia na wahanga wa janga la Hillsborough (Hillsborough Family Support Group -HFSG) wataungana leo katika maadhimisho ya kuwakumbuka wapendwa wao waliofariki tarehe kama ya leo miaka 28 iliyopita wakiwa uwanjani. Tukio hilo maarufu kama "HILLSBOROUGH DISASTER 96" lilitokea katika mchezo wa nusu fainali ya mwaka 1988-1989 kati ya Liverpool na Nottingham Forest katika uwanja wa Hillsborough .Katika tukio hili watu 96 walifariki dunia na wengine 766 kujeruhiwa na kuacha kumbukumbu mpaka leo yakuwa ni janga kubwa la kimichezo kuwahi kutokea katika hisporia ya michezo Uingereza. Chanzo cha tukio hili ni amri ya kimakosa ya Afisa polisi ambaye ni mkuu wa siku hiyo Police David Duckenfield iliyoamuru geti la kuingia uwanjani lililojulikana kama Geti "C" kufunguliwa angali nje kulikuwa na idadi kubwa ya mashabiki waliokuwa wakishinikiza kuingia ndani. Baada ya geti hi...

TIMU YA LIGI DARAJA LA KWANZA UINGEREZA YAPANDA DARAJA KWA MARA YA KWANZA

Brighton & Hove Albion imefanikiwa kupanda daraja na hivyo kushiriki ligi kuu ya uingereza msimu ujao baada ya kujikusanyia jumla ya point 79 katika michezo 43 iliyokwisha cheza mpaka sasa ikiwa imesalia michezo 3. Brighton Albion inayonolewa na kocha wa zamani wa Birmingham City na Norwich City, Chris Hughton  itakuwa ni timu ya 48 kushiriki ligi kuu ya uingereza baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wigan Athletics siku ya jumatatu. Kwa upande wake kocha Hughton amesema kuwa anajivunia namna ambavyo timu hiyo walivyojirudi kwa kasi kufuatia hali ya msimu. Aidha ameongeza kuwa kuweka nguvu zao kwa pamoja hadi kufikia hatua hii sio jambo rahisi, na wanahitaji kila aina ya pongezi. Brighton walinusa nafasi ya kucheza ligi kuu ya uingereza msimu uliopita baada ya kuwa katika ushindani mkubwa na kujikuta wakipoteza nafasi hiyo kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga dhidi ya Barnely kufuatia matokeo ya sare waliyoyapata dhidi Middlesbrough. Kufuatia ushindi huu ...